Ajali ya Treni ya SGR: TRC Yathibitisha Tukio, Wataalamu kufika Kwenye Eneo la Ajali
Msemaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Ndugu Fredy Mwanjala amethibitisha kupokea taarifa za ajali ya treni kupitia mawasiliano na moja ya vyombo vya habari kwa njia ya simu. Amesema, “tumepokea hizo taarifa za treni kupata ajali na kwa kuwa ndio kwanza tumezipata kwa sasa Mkurugenzi Mkuu na Katibu Mkuu wa Wizara wote tunaelekea eneo la tukio na tunatoa taarifa baadaye baada ya kufanya tathmini ya kina na Wataalamu.”
Wananchi wametakiwa kuwa watulivu huku taarifa kamili ikisubiriwa kutoka mamlaka husika baada ya uchunguzi wa kina.