Ajali ya Treni ya Mwendo Kasi SGR - TRC Yathibitisha Tukio, Wataalamu kufika Kwenye Eneo la Ajali

Shirika la Reli Tanzania (TRC) limethibitisha kupokea taarifa za ajali ya treni, huku Mkurugenzi Mkuu na Katibu Mkuu wa Wizara wakielekea eneo la tukio kwa uchunguzi wa kina. Msemaji wa TRC, Ndugu Fredy Mwanjala, amesema taarifa rasmi zaidi zitatolewa baada ya tathmini kamili kufanyika.

Ajali ya Treni ya SGR: TRC Yathibitisha Tukio, Wataalamu kufika Kwenye Eneo la Ajali

Msemaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Ndugu Fredy Mwanjala amethibitisha kupokea taarifa za ajali ya treni kupitia mawasiliano na moja ya vyombo vya habari kwa njia ya simu. Amesema, “tumepokea hizo taarifa za treni kupata ajali na kwa kuwa ndio kwanza tumezipata kwa sasa Mkurugenzi Mkuu na Katibu Mkuu wa Wizara wote tunaelekea eneo la tukio na tunatoa taarifa baadaye baada ya kufanya tathmini ya kina na Wataalamu.”

Wananchi wametakiwa kuwa watulivu huku taarifa kamili ikisubiriwa kutoka mamlaka husika baada ya uchunguzi wa kina.

Makala zinazofanana

Hakuna makala zinazofanana kwa sasa.

Image

Umenisoma Blog

Follow Umenisoma for community well-being. - Fuatilia umenisoma kwa ustawi wa jamii

Tafuta