Tangazo la Nafasi za Kazi TAKUKURU (Nafasi 500) - Aprili 2026
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) anawatangazia Watanzania wenye sifa kuomba kuajiriwa katika nafasi za kazi kwa ajili ya ofisi za TAKUKURU Wilaya. Tangazo hili limechapishwa rasmi tarehe 11 Aprili 2026.
1.0 AFISA UCHUNGUZI (NAFASI 250)
1.1 Sifa za Kitaaluma:
Muombaji awe na angalau elimu ya shahada ya kwanza iliyotolewa na chuo kinachotambulika na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika moja ya fani zifuatazo:
- Uhasibu, Usanifu Majengo, Usimamizi wa Biashara, Ukadiriji wa Majengo (Quantity Surveying), Uhandisi wa Usindikaji wa Kemikali, Maendeleo ya Jamii.
- Sayansi ya Kompyuta/TEHAMA, Uhandisi wa Ujenzi, Uchumi na Mipango, Uhandisi wa Umeme, Lishe na Sayansi ya Chakula.
- Usimamizi wa Rasilimali Watu, Usimamizi na Tathmini ya Ardhi, Sheria, Uhandisi wa Mitambo, Uhandisi wa Mafuta na Gesi.
- Ununuzi na Ugavi, Usimamizi wa Miradi, Ushauri Nasaha, Utawala wa Umma, Mahusiano ya Umma/Mawasiliano ya Umma.
- Usimamizi wa Kumbukumbu, Sayansi ya Michezo/Elimu ya Viungo, Takwimu, na Uhandisi wa Maji.
Zingatia:
- Muombaji awe na ufaulu wa kuanzia daraja la pili la chini (Lower Second Class).
- Waombaji waliosajiliwa na Bodi za Kitaaluma watapewa kipaumbele zaidi.
1.2 Sifa zingine:
- Waombaji wasiwe wamefika umri wa miaka 29 kufikia Mei, 2026.
2.0 MCHUNGUZI MSAIDIZI (NAFASI 250)
2.1 Sifa za Kitaaluma:
Awe na angalau cheti au astashahada kutoka kwenye shule/vyuo vinavyotambulika na serikali kwenye moja kati ya fani zifuatazo:
- Ulinzi (Security Skills): Lazima awe na “Basic Technical Certificate/Technical Certificate /Diploma in Wildlife Management and Law Enforcement, au Basic Peoples Militia Training” (Mgambo) kutoka taasisi inayotambuliwa Tanzania, pamoja na uzoefu katika ulinzi.
- Ufundi wa Magari / Panel Beating / Upakaji Rangi: Cheti cha NVA/NTA Ngazi ya 3–4, pamoja na uzoefu na ujuzi wa vitendo.
- Ujuzi wa Udereva (Madereva Daraja “C”): Leseni halali ya udereva Daraja C, rekodi safi ya udereva, na uzoefu unaothibitika.
- Huduma kwa Wateja / Msaidizi wa Ofisi: Cheti katika fani yoyote, uzoefu wa kuhudumia wateja na kusaidia shughuli za ofisi.
- Msaidizi wa Uhasibu: Diploma inayotambuliwa katika fani ya uhasibu na uelewa wa taratibu za fedha za umma.
- Masomo ya Ukatibu (Katibu Muhtasi): Diploma ya ukatibu muhtasi, umahiri wa usimamizi wa ofisi na TEHAMA.
- Fundi wa Kompyuta: Cheti au diploma ya ufundi katika matengenezo ya kompyuta (hardware, mitandao, na software).
- Fundi wa Mashine za Ofisi: Mafunzo ya kiufundi ya kufunga na kufanya matengenezo ya Printer, Photocopier, na Scanner.
2.2 Sifa zingine:
- Mwombaji ni lazima awe raia wa Tanzania.
- Umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 25.
3.0 MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI WOTE
- Mwombaji lazima awe mtu mwenye uadilifu wa hali ya juu.
- Asiwe na rekodi yoyote ya uhalifu.
- Awe tayari kufanya kazi katika wilaya yoyote ya Tanzania Bara.
- Lazima awasilishe nakala za vyeti halisi zilizothibitishwa (Certified copies). Atakayewasilisha vyeti vya kughushi atachukuliwa hatua za kisheria.
- Mtu aliyefukuzwa au kuachishwa kazi serikalini kwa sababu yoyote hastahili kuomba.
- Mtumishi wa Umma lazima apitishe maombi yake kwa mwajiri wake.
- Nyaraka za kuambatisha (zilizothibitishwa):
- Vyeti vya Shahada/Stashahada ya Juu na Nakala ya Matokeo ya Masomo (Transcripts).
- Vyeti vya Kidato cha IV na Kidato cha VI.
- Cheti cha Darasa la Saba.
- Vyeti vya Kitaalamu (pale inapohusika) na Cheti cha Kuzaliwa.
- Vyeti vya nje ya nchi lazima vithibitishwe na mamlaka husika (TCU, NACTVET, NECTA).
- Kuambatisha Wasifu (CV) yenye uzoefu wa kazi, anuani, baruapepe, na namba ya simu.
- Majina na mawasiliano ya wadhamini (referees) watatu waaminifu.
- Kitambulisho cha Taifa (NIDA) au namba ya NIDA ni lazima.
- Barua za uthibitisho, slipu za matokeo, au nakala za matokeo hazitakubaliwa.
- Barua ya maombi lazima iandikwe kwa mkono (Kiswahili au Kiingereza).
- Maombi yasiyo na nyaraka zote hayatazingatiwa.
- Watakaopita mchujo wa awali tu ndio watakaojulishwa.
4.0 JINI YA KUWASILISHA MAOMBI
Maombi yote yatumwe kupitia mfumo wa kielekitroniki wa ajira wa TAKUKURU: ajira.pccb.go.tz na si vinginevyo. Maombi ya posta au mkono hayatapokelewa.
Barua za maombi ya ajira ziandikwe kwa Anuani:
Mkurugenzi Mkuu,Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa,
Mtaa wa Jamhuri, S.L.P. 1291,
1101 DODOMA.
MWISHO WA KUTUMA MAOMBI: Tarehe 03 Mei, 2026.